Welcome/Karibu sana!

Karibu sana/Welcome!

We provide an inspirational forum for people with challenges in life,businesses,education etc to exchanges ideas and share the solutions to the globe.We are mainly focused on youths who are especially facing many challenges in life.Mobile no:+255653259644

Looking for something?

Subscribe to this blog!

Receive the latest posts by email. Just enter your email below if you want to subscribe!

Friday, 16 October 2015

NEC:VYAMA VYA SIASA ACHENI KUTOA TAARIFA ZA UONGO

NEC yavionya vyama         vya  siasa kuacha kutoa taarifa za     uongo kwa wafuasi                     wao.
Tume ya taifa ya uchaguzi (NEC) imevionya vyama vya siasa kuacha kutoa taarifa za uongo kwa wafuasi wao dhidi ya tume hiyo na badala yake watoe taarifa sahihi kuhusu tume na kujikita kuwaelimisha wafuasi wao na wananchi kujitokeza kupiga kura Oktoba 25 mwaka huu.
Onyo hilo limetolewa na kamishna wa tume hiyo Bi. Mary Longway wakati akizungumza na viongozi wa vyama vya siasa na watendaji wa tume hiyo mjini Songea mkoani Ruvuma.
 Kamishna huyo amesema kama vyama vya siasa vitawahamasisha wafuasi wao kubaki kwenye vituo vya kupigia kura kutakuwa na uwezekano wa kutokea vurugu zitakazowatisha wapiga kura kujitokeza kupiga kura huku kaimu mwenyekiti wa Chadema mkoani Ruvuma Bw. Rashid Chitepete akisema ni lazima wawe jirani na vituo vya kupigia kura ili kuwepo na watu wa kuwatangazia matokeo.Naye kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma ACP Mihayo Msikhela amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuhubiri amani  kwa wafuasi wao

No comments :

Post a Comment