Kwa mujibu wa uanishaji uliofanywa na wataalamu wa Shirika la Afya
Duniani yaani WHO, kuna hatua kuu nne za ugonjwa wa VVU/UKIMWI ambazo
ni:
1. Hatua ya kwanza au maambukizi ya mwanzo ya HIV. Hatua hii huwa ni
ya muda wa wiki nne na ni asilimia 20 tu ya watu wenye maambukizi ya VVU
walio kwenye hatua hii ambao hupata dalili na viashiria vikali vya
ugonjwa huu, lakini mara nyingi madaktari hushindwa kutambua kama
mgonjwa amepata maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutokana na dalili na
viashiria vyake kufanana sana na dalili za magonjwa mengine. Mgonjwa
aliye katika hatua hii ya kwanza ya maambukizi ya VVU huweza kuonesha
dalili na viashiria kama vile kuvimba tezi, kupatwa na homa kali, kuumwa
koo, kujihisi mchovu, kujihisi maumivu sehemu mbalimbali mwilini
kutokwa na vipele mwilini,kutapika, kuharisha au kuumwa tumbo Endelea hapa...
No comments :
Post a Comment