Welcome/Karibu sana!

Karibu sana/Welcome!

We provide an inspirational forum for people with challenges in life,businesses,education etc to exchanges ideas and share the solutions to the globe.We are mainly focused on youths who are especially facing many challenges in life.Mobile no:+255653259644

Looking for something?

Subscribe to this blog!

Receive the latest posts by email. Just enter your email below if you want to subscribe!

Wednesday, 21 October 2015

Netanyahu(waziri mkuu wa Israel):"Haj Amin al Husseini alimshauri hitler awateketeze wayahudi"

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amekosolewa baada ya kudai kuwa kiongozi wa kidini mpalestina alimshawishi aliyekuwa kiongozi wa kimila wa Ujerumani Adolf Hitler kutekeleza maauaji ya kimbari ya wayahudi.
Kiongozi mkuu wa kidini mjini Jerusalem Haj Amin al Husseini kwa muda mrefu amekuwa akituhumiwa kuwa anaunga mkono mauaji ya kimbari ya wayahudi.
Lakini katika hotuba yake kwenye mkutano wa kimataifa wa wayahudi, bwana Netanyahu ameendeleza shutuma hizo.
Kulingana naye, Hitler alitafuta maoni kutoka kwa kiongozi huyo wa kidini kuhusiana na ari yake ya kuwafurusha wayahudi barani Ulaya.
Kwa maelezo yake Netanyahu, kiongozi huyo alimwambia Hitler kuwa wayahudi wote wangeenda Palestina iwapo angewafukuza Ulaya.
Na Hitler alipomuuliza,afanye nini ?
Netanyahu, anasema kuwa kiongozi huyo alimshauri Hitler "awateketeze wayahudi"
Wataalam wa maswala ya historia hata hivyo wamekuwa wakipuuzilia mbali madai hayo kuwa siyo ya kweli.
Viongozi wa upinzani nchini Israel wametaja madai ya Netanyahu kama historia ya kupotosha.
Viongozi wa kipalestina kwa upande wao wamesema matamshi hayo yanaonyesha jinsi Waziri huyo mkuu wa Israeli anawachukia wapalestina.

No comments :

Post a Comment