Welcome/Karibu sana!

Karibu sana/Welcome!

We provide an inspirational forum for people with challenges in life,businesses,education etc to exchanges ideas and share the solutions to the globe.We are mainly focused on youths who are especially facing many challenges in life.Mobile no:+255653259644

Looking for something?

Subscribe to this blog!

Receive the latest posts by email. Just enter your email below if you want to subscribe!

Wednesday, 21 October 2015

Kenyatta aipuuza mahakama ya ICC

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amepuzilia mbali onyo la jaji wa mahakama ya ICC Chile Eboe-Osuji ya kuwataka wakenya wakome kuijadili kesi inayoendelea kusikizwa dhidi ya Naibu Rais wa Kenya William Ruto na mwandishi wa habari Joshua Sang.
Jaji Eboe alionya wanasiasa wanaoitukana mahakama hiyo hususan katika mikutano ya hadhara ya maombi ambayo imetia fora nchini Kenya.
Akilihutubia taifa katika hafla ya kuadhimisha sikukuu ya mashujaa, Rais Kenyatta amesema
''hata wale wanaotusukumie hii mambo ya icc kila siku mambo ni ICC wawachane na sisi wawache sisi tuendeleee kujenga na kuunganisha wakenya wenzetu.''
''Na sisi wakenya tuendelee kuomba jaji fulani hawezi kutuambia ati sisi hatuna nguvu ya kuomba ... sisi tunaamini mungu, Na sisi tunauhuru wa kuomba, Na tutaendelea na maombi kwa sababu tunajua maombi faida yake ni nini'."
Uhuru alisema akiashiria onyo la Jaji Chile Eboe-Osuji anayesikiza kesi dhidi ya Ruto na Sang.
Kenyatta alisema kuwa mikutano ya maombi ya kumuombea naibu wake itaendelea.
Naibu wake William Ruto na muandishi habari Joshua arap Sang wanakabiliwa na tuhuma za kuchochea mapigano yaliyosabisha vifo vya watu 1,300 huku wengine laki sita wakihamishwa makwao punde baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2007 kutangazwa nchini Kenya.''
Jaji

No comments :

Post a Comment