Welcome/Karibu sana!

Karibu sana/Welcome!

We provide an inspirational forum for people with challenges in life,businesses,education etc to exchanges ideas and share the solutions to the globe.We are mainly focused on youths who are especially facing many challenges in life.Mobile no:+255653259644

Looking for something?

Subscribe to this blog!

Receive the latest posts by email. Just enter your email below if you want to subscribe!

Wednesday, 21 October 2015

UKAWA wastopisha kampeni,mazishi ya Dk Makaidi.

Aliyekuwa mwenyekiti mwenza wa chama cha UKAWA nchini Tanzania, Dkt. Emmanuel Makaidi ambaye aliaga dunia siku tano zilizopita, alizikwa Jumanne mjini Dar es Salaam.
Marehemu Makaidi alikuwa pia mwenyekiti wa chama cha National League and Democrasy NLD, mojawapo ya vyama vilivyoungana kuanzisha chama kikuu cha upinzani, UKAWA, kinachoongozwa na aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowasa.
Upinzani ulisitisha kampeni kwa muda wa saa 24 kutoa heshima za mwisho kwa kiongozi huyo.
Viongozi wa tabaka mbali mabli walihudhuria mazishi hiyo katika makaburi ya Sinza mjini Dar es Salaam.
Makaidi alitarajiwa kugombea kiti cha ubunge katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika siku ya Jumapili.
Kufikia sasa wagombea sita waliotarajiwa kuwania viti vya ubunge katika uchaguzi huo wameaga dunia

No comments :

Post a Comment