Welcome/Karibu sana!

Karibu sana/Welcome!

We provide an inspirational forum for people with challenges in life,businesses,education etc to exchanges ideas and share the solutions to the globe.We are mainly focused on youths who are especially facing many challenges in life.Mobile no:+255653259644

Looking for something?

Subscribe to this blog!

Receive the latest posts by email. Just enter your email below if you want to subscribe!

Wednesday, 21 October 2015

Urusi na Marekani wakubaliana kutoshambulia kwa ndege Syria

Urusi na Marekani zimetia saini makubaliano yanayotarajiwa kuzuia ndege za kijeshi za nchi hizo kushambuliana nchini Syria.
Habari za kutiwa saini kwa mkataba huo zimethibitishwa na maafisa kutoka nchi zote mbili.
Urusi ilianza kushambulia kwa ndege maeneo ya Syria Septemba 30, ikisema ilikuwa ikiwalenga wapiganaji wa kundi la Islamic State (IS).
Wiki iliyopita, Marekani ilisema ndege za mataifa hayo zilikuwa “zimeingia eneo moja ya mapigano” na zilikuwa karibu sana kukutana.
Maafisa wa mataifa hayo wamekuwa wakitafuta mwafaka tangu mwishoni mwa mwezi Septemba.
Msemaji wa Pentagon Peter Cook amesema maelezo zaidi kuhusu makubaliano hayo yatasalia kuwa siri, kufuatia ombi la Urusi.
Hata hivyo, alisema mwafaka huo unaweka mikakati ya pande zote mbili kuwasiliana.
Nchi hizo mbili hata hivyo hazitaelezana habari za kijasusi kuhusu maeneo yanayolengwa na wanajeshi wa kila upande.
Bw Cook alisema mkataba huo unahakikisha ndege za kila taifa zitakaa “umbali salama” kutoka kwa ndege za taifa hilo jingine. Hata hivyo, hakueleza umbali ulioafikiwa.
Wiki iliyopita, Pentagon ilisema ndege za kijeshi za Urusi na Marekani wakati mmoja zilikuwa zimekaribiana kiasi cha marubani kuweza kuonana, kilomita 15 hadi 30.
Waziri msaidizi wa ulinzi wa Urusi Anatoly Antonov amesema makubaliano hayo yameweka mikakati ya kuzuia kushambuliana kwa ndege za Marekani na Urusi.

No comments :

Post a Comment