Welcome/Karibu sana!

Karibu sana/Welcome!

We provide an inspirational forum for people with challenges in life,businesses,education etc to exchanges ideas and share the solutions to the globe.We are mainly focused on youths who are especially facing many challenges in life.Mobile no:+255653259644

Looking for something?

Subscribe to this blog!

Receive the latest posts by email. Just enter your email below if you want to subscribe!

Wednesday, 21 October 2015

Chelsea washindwa kutamba Ulaya

Chelsea walitoka sare tasa mechi yao ya tatu katika Kundi G kwenye mechi ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ugenini dhidi ya Dynamo Kiev.
Vijana hao wa Jose Mourinho waligonga mlingoti wa goli mara mbili na pia wakanyimwa penalti.
Eden Hazard alikaribia sana kufunga, lakini kipa Oleksandr Shovkovskiy akagongesha mpira wake kwenye mlingoti.
Winga wa Dynamo Kiev Andriy Yarmolenko alishambulia sana kutoka kulia lakini aliishia kupokonywa mpira. Alipokonywa mpira mara 25 kwenye mechi hiyo.
Chelsea walifaa kupewa penalti baada ya Cesc Fabregas kuanguka alipokabiliwa vikali na Serhiy Rybalka lakini refa hakusikia kilio chao.
Frikiki ya Willian iligonga mwamba wa goli kabla ya Asmir Begovic kumzuia mchezaji mwenyeji Derlis Gonzalez kuwafunga Chelsea kwenye mechi hiyo iliyochezewa Ukraine.
Vijana hao wa Mourinho sasa wameshinda mechi moja pekee kati ya tano walizocheza majuzi zaidi katika mashindano yote.
Hata hivyo, uchezaji wao ulionekana kuimarika pakubwa Ulaya tangu walipolazwa na Porto Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya 2-1 ugenini Septemba 29.
Ushindi wa Porto 2-0 dhidi ya Maccabi Tel-Aviv unawafanya Chelsea kusalia nambari tatu kundini wakiwa na alama nne, moja nyuma ya Kiev na alama tatu nyuma ya viongozi wa kundi Porto

No comments :

Post a Comment