Welcome/Karibu sana!

Karibu sana/Welcome!

We provide an inspirational forum for people with challenges in life,businesses,education etc to exchanges ideas and share the solutions to the globe.We are mainly focused on youths who are especially facing many challenges in life.Mobile no:+255653259644

Looking for something?

Subscribe to this blog!

Receive the latest posts by email. Just enter your email below if you want to subscribe!

Wednesday, 21 October 2015

KIKWETE akabidhi magari 399 kwa jeshi la polisi kwaajili ya uchaguzi!!

Rais Kikwete amemkabidhi IGP Mangu funguo za magari hayo katika Chuo Kikuu cha Mafunzo ya Polisi Kurasini jijini Dar es salaam katika sherehe ya kukabidhi magari 399 kati ya 777 yanayoletwa kwa ajili ya kusaidia utendaji kazi wa jeshi la polisi
Rais JAKAYA KIKWETE ameliagiza Jeshi la Polisi nchini kuendelea kufanya kazi kwa weledi kama ilivyokuwa wakati huu wa kampeni za uchaguzi ili kuhakikisha Taifa linamaliza uchaguzi Mkuu kwa amani na utulivu.
Rais KIKWETE ametoa agizo hilo Jijini DSM wakati wa akikabidhi magari 399 ya jeshi la polisi ikiwa ni utekelezaji wa programu ya maboresho kwa Jeshi la Polisi  nchini. 
Kwa mujibu wa Rais KIKWETE, katika kipindi hiki ambapo kampeni za uchaguzi mkuu ujao zinaelekea kumalizika, Jeshi la polisi nchini limefanya kazi nzuri katika kulinda raia na mali zao.
Magari hayo 399 yaliyokabidhiwa na Rais KIKWETE ni miongoni mwa Magari 777 yaliyoombwa na Jeshi la Polisi nchini kwa ajili ya kufanya kazi ya kulinda raia pamoja na mali zao. 
Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi MATHIAS CHIKAWE ametoa wito kwa Watendaji wa Jeshi la Polisi nchini kuyatumia magari hayo kwa malengo yaliyokusudiwa.

No comments :

Post a Comment