Welcome/Karibu sana!

Karibu sana/Welcome!

We provide an inspirational forum for people with challenges in life,businesses,education etc to exchanges ideas and share the solutions to the globe.We are mainly focused on youths who are especially facing many challenges in life.Mobile no:+255653259644

Looking for something?

Subscribe to this blog!

Receive the latest posts by email. Just enter your email below if you want to subscribe!

Wednesday, 21 October 2015

PINDA ayataka makampuni ya ujenzi kujenga magorofa

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifungua pazia kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengoa makazi na biashara la Cictoria Place linalojengwa na NHC katika eneo la Victoria jijini Dar es salam Octoba 20,2015. Kushoto ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela kairuki na kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu
Waziri mkuu MIZENGO PINDA ameyataka mashirika na kampuni za ujenzi nchini kujenga nyumba za makazi zenye ghorofa ndefu ili watanzania wengi wapate fursa ya kupata nyumba. 
Akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba za ghorofa pacha za Victoria place unaofanywa na shirika la nyumba – NHC- jijini DSM, PINDA amesema ujenzi shadidi unahusisha nyumba za gorofa ndefu ambao hutumia eneo dogo na hivyo hupunguza matumizi makubwa ya ardhi. 
Nae Mkurugenzi Mkuu wa NHC, NEHEMIA MCHECHU  amesema ujenzi wa nyumba hizo utagharimu shilingi bilioni 30.3 na utahusisha nyumba za makazi 88, eneo la kuegeshea magari na maduka makubwa.

No comments :

Post a Comment